Thu, 20 Jul 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Simba imethibitisha kukamilisha usajili wa kiungo wa kati, Abdallah Hamisi Riziki (25) raia wa Tanzania kwa kandarasi ya miaka miwili akiwa Mchezaji huru.
Abdallah amewahi pia kuhudumu katika Vilabu vya Muhoroni FC, SoNy Sugar, Bandari FC zote za Kenya na Opara United ya Botswana.
Abdallah ndiye anatajwa kuwa mrithi wa Jonas Mkude aliyetimkia Yanga baada ya kumaliza mkataba wake na Simba aliyoitumikia kwa miaka 13.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: