Baada ya kuzungumzwa mengi kwa takribani siku nzima ya leo juu ya mustakabali wa kiungo fundi wa Simba SC Clatous Chama kuwa yuko mbioni kuondoka klabuni hapo.
Sasa Klabu ya Simba kupitia kwa Meneja wa habari na Mawasiliano wa Klabu ya Simba SC Ahmed Ally umetoa kauli kuhusiana na sakata hilo.
Ahmed Ally kupitiua ukurasa wake rasmi wa Twitter ameandika;
"Kumekua na sintofahamu kuhusu mkataba wa Mwamba wa Lusaka kiasi cha kuzua taharuki miongoni mwa mashabiki wetu
Taarifa ni kwamba Chama bado ana mkataba na Simba kwa muda wa mwaka mmoja hadi 2024
Hatujapokea ofa kutoka klabu yeyote ikihitaji kumnunua Chama
Na wala hatujapokea maombi ya mchezaji kutaka kuvunja mkataba
Mchezaji yeyote ambae tunamhitaji atabaki kuitumikia Simba kulingana na mahitaji ya mkataba wetu"
Imesomeka taarifa ya Ahmed Ally, lakini je ina ukweli au tumsubiri na mchezaji atazungumza nini? Tuachie maoni yako