Wakati Klabu ya Yanga ikihitimisha kilele cha "Siku ya Mwananchi" leo Julai 22 kuna mambo mengi ambayo Wanayanga wanatarajia kuyaona katika siku hii muhimu kwa klabu ya Yanga.
Miongoni mwa mambo mengi yaliyopa katika siku hii ni utambulisho wa Wachezaji watakaoitumika Klabu ya Yanga kwa msimu ujao 2023/24.
Bila kusahau utambulisho wa sajili za wachezaji wapya zilizofanywa na Klabu ya Yanga.
Sasa katika Utambulisho wa leo Afisa habari wa Yanga, ametamba kuwa wananchi wanapaswa kuja kwa wingi Uwanjani kwani ni siku ya kumbatiza kiungo wao mpya Jonas Mkude almaarufu kama "Nungunungu"
Ally Kamwe amesema sikiu ya leo wanapa jina jipya Mkude kutoka lile la awali Nungunungu na kuitwa Casemiro kwani uwezo wa Mkude ni wa hali ya juu katika nafasi ya kiungo cha ulinzi