Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ahmed: Baleke bado yupo sana Msimbazi

Baleke X Ibenge Baleke bado yupo sana Msimbazi

Mon, 15 May 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Meneja Habari na Mawasiliano wa Simba Sc, Ahmed Ally kupitia kipindi cha #SportsArena ya #WasafiFm amethibitisha kuwa Baleke ni mchezaji halali wa Simba kwa kandarasi ya miaka miwili.

“Baleke ni Mshambuliaji wa Simba amesaini kandarasi ya kuitumikia Simba kwa muda wa miaka miwili, TP Mazembe walipewa pesa yao na ametumikia kandarasi yake miezi minne tu.

“Niwatoe shaka wana Simba ya kwamba Baleke bado yupo sana Simba kwa muda mwingine, mpaka sasa hakuna ofa yoyote kutoka klabu yoyote ikimuulzia Baleke.

“Manula bado anamkataba wa miaka miwili na Simba, bado yupo sana, Mohammed Hussein hana popote pa kwenda duniani zaidi ya Simba,” Meneja Habari na Mawasiliano wa Simba Sc, amesema Ahmed Ally.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: