Mwili wa kijana Dominick Kigula (31) aliyeuwawa kwa kuchomwa kisu yeye pamoja na anayedaiwa kuwa ni mpenzi wake Esther Shiyago (25) umezikwa jana Julai 22, 2022 katika makaburi ya Sechelela yaliyopo kata ya Makulu Dodoma.
Wawili hao waliuawa alfajiri ya Jumatano, Julai 20, 2022 wakiwa kwenye nyumba aliyopanga Dominick mtaa wa Msangalee, kata ya Dodoma Makulu jijini Dodoma huku chanzo kikidaiwa kuwa ni wivu wa mapenzi.
Mtuhumiwa wa mauaji hayo anadaiwa kuwa ni kijana mmoja aliyekuwa kwenye mahusiano na Esther na bado anaendelea kusakwa na Jeshi la Polisi.
Marehemu Dominick aliyekuwa akifanya shughuli za kuendesha bodaboda ameacha mtoto wa miaka minne ambaye alikuwa amezaa na mwanamke mwingine aliyewahi kuwa naye hapo awali.