Ukiachia Watu zaidi ya 60 waliofariki kutokana na maporomoko ya tope Katesh, Wilayani Hanang Mkoani Manyara, wapo walionusurika vifo akiwemo Enock ambaye anakiri kama sio mkia wa ng’ombe alioushika basi inawezekana sasa hivi Ndugu zake wangekua wakiongea habari nyingine.
Ukiachia Watu zaidi ya 60 waliofariki kutokana na maporomoko ya tope Katesh, Wilayani Hanang Mkoani Manyara, wapo walionusurika vifo akiwemo Enock ambaye anakiri kama sio mkia wa ng’ombe alioushika basi inawezekana sasa hivi Ndugu zake wangekua wakiongea habari nyingine. “Mimi sikulala nyumbani sababu kulikuwa na wageni tulikuwa na sherehe ikabidi nikalale kwa jirani ndipo maporomoko yaliponikuta, tuliangukiwa na ukuta halafu tukasombwa tukashuka mpaka huko chini nikakutana na ng’ombe nikamshika mkia akanivuta nikatoka kwenye tope,” anasimulia Enock.