Swaumu Abdala (13) ambaye ni mwanafunzi wa darasa la sita katika shule ya msingi Bugongwa mtaa wa Igombe B kata ya Bugogwa halmashauri ya manispaa ya Ilemela amepoteza maisha baada ya kupigwa na radi wakati akikinga maji na kucheza kwenye mvua na wenzake jirani na nyumbani kwao.
Ndugu wa mtoto huyo wamesema wakati tukio hilo likitokea marehemu na wenzake walikuwa wakichota maji na kucheza kwenye mvua ndipo mtoto huyo mmoja alipo pigwa radi.
Mganga mfawidhi wa kituo cha afya cha Karume Dk Thomas Shija akithibitisha kutokea kwa kifo hicho amesema walimpokea mtoto huyo siku ya jumamosi majira ya saa tano akiwa amefariki.