Thu, 23 Mar 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Diwani wa kata ya Tandika Manispaa ya Temeke Dar es Salaam, Uzahiri Athuman amethibitisha kutokea kwa kifo cha mtoto wa miaka 5 aliyetumbukia kwenye shimo la maji taka kilitokea jana Machi 22, 2023.
Diwani amesema mtoto huyo alipoteza Maisha wakati zoezi la kumuokoa likiendelea ametoa wito kwa wananchi kufunika mashimo ya choo kwa zege ili kujiepusha na matukio kama hayo.
Aidha ameziagiza kamati za afya kupitia nyumba za mtaa huo kuhakikisha mashimo ya vyoo ambayo yako wazi kufunikwa.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: