Jeshi la polisi Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma linamshikilia kijana mmoja anayejulikana kwa jina la David Ruya, mkazi wa Tunduru mjini kwa tuhuma za kukutwa na binti wa miaka 12 ambaye ni mwanafunzi, akiwa chumbani kwa kijana huyo majira ya saa tano usiku.
Kwa mujibu wa Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Julius Mtatiro anasema alipata taarifa za kuwepo kwa tukio hilo kutoka kwa vyanzo vyake vya kuaminika na baada ya kufika eneo la tukio akiwa na polisi, mtuhumiwa alikutwa chumbani kwake huku mtoto akiwa ametoka nje akiwa na simu ya kijana huyo.
Jeshi la Polisi mkoani humo linawashikilia binti na kijana huyo kwa uchunguzi zaidi ili sheria ichukue mkondo wake.