Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea, Mohamed Hassan Moyo ameamuru kuvunjwa kwa baadhi ya madarasa ya Shule ya Msingi Majogo katika Kijiji cha Litula Kata ya Marambo kutokana na uchakavu wa majengo ya Shule hiyo ambayo yanahatarisha maisha ya Wanafunzi na Walimu.
Akiwa katika ziara ya Kijiji kwa Kijiji yenye kauli mbiu isemayo "ulipo nipo toa kero yako sema kweli sio majungu", DC huyo amefanikiwa kufika katika Shule hiyo na kuikuta ikiwa katika hali ya uchakavu mkubwa wa majengo ambayo yanahatarisha maisha ya Wanafunzi na Walimu.
Moyo amesema haiwezekani Wanafunzi wakaendelea kusoma kwenye madarasa ambayo yamejawa na nyufa kila kona hivyo madarasa hayo yabomolewe haraka iwezekanavyo.
Amemtaka Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea kujenga upya madarasa hayo ili Wanafunzi wa Kijiji cha Majogo waendelee kupata elimu inavyotakiwa kwa faida ya Taifa.