Mahakama nchini Marekani hatimae imewakuta maafisa watatu wa polisi wa zamani wa Minneapolis na hatia ya kukiuka haki za kiraia za George Floyd. Tou Thao, J. Alexander Kueng, na Thomas Lane walishtakiwa kwa kumnyima Floyd haki yake ya matibabu wakati Afisa Derek Chauvin alipomkandamiza kwa goti shingoni George Floyd kwa zaidi ya dakika tisa alipokuwa amefungwa pingu barabarani mnamo Mei 25, 2020.
Polisi hao Thao na Lane pia walishtakiwa kwa kukosa kuingilia kati kumzuia Chauvin katika Mauaji hayo ambapo Kueng alipiga magoti kwenye mgongo wa Floyd, Lane alishikilia miguu yake na Thao akawazuia waliokuwa karibu.
Chauvin alipatikana na hatia ya mauaji mwaka jana katika mahakama ya serikali na kuhukumiwa miaka 22.5.