Mon, 16 May 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Baada ya watu 10 kuuawa katika shambulio linalotajwa kuwa la kibaguzi huko Buffalo Jijini New York, Mamlaka zimesema Mtuhumiwa aliwekwa kizuizini mwaka 2021 na kufanyiwa tathmini ya Afya ya Akili alipotoa kitisho Shuleni.
Payton Gendron (18) alijisalimisha Polisi baada ya kufyatulia risasi watu 13, ikielezwa 11 kati yao walikuwa Weusi. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres amelaani mauaji hayo akisema ni itikadi kali ya ubaguzi wa rangi.
Meya wa Buffalo, Byron Brown amesema Mtuhumiwa huyo alidhamiria kuua watu weusi wengi.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: