Polisi Dodoma wanamshikilia Joachim Joseph mkazi wa Arusha kwa kusafirisha Wahamiaji 16 wasio na vibali ambao ni Raia wa Ethiopia wakitokea mkoa wa Kilimanjaro kuelekea mkoa wa Mbeya ili kuwavusha mpaka kelekea Afrika kusini.
Polisi Dodoma wanamshikilia Joachim Joseph mkazi wa Arusha kwa kusafirisha Wahamiaji 16 wasio na vibali ambao ni Raia wa Ethiopia wakitokea mkoa wa Kilimanjaro kuelekea mkoa wa Mbeya ili kuwavusha mpaka kelekea Afrika kusini. Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma kamishna Msaidizi wa Polisi Martin Otieno amesema Dereva huyu amekamatwa akiwa na gari aina ya Landcruser namba T 752 BVL lakini alitumia mbinu ya kufunga namba za Shirika la Umma ambazo ni SU 35970 ili asishtukiwe au kusimamishwa barabarani.