Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Dr Nandipha atoa mpya "Thabo Bester alikuwa ameniteka"

Dr Nandipha Dr Nandipha na Bester

Mon, 17 Apr 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Taarifa zinaeleza kuwa kuwa Dokta Nandipha Magudumana awali aliiambia mamlaka ya Tanzania kuwa anashikiliwa kinyume na matakwa yake na Thabo Bester, muuaji na mbakaji hatari wa wanawake nchini Afrika Kusini.

Bester, alidanganya kifo chake kwa usaidizi wa Magudumana kumficha alipotoroka jela, Mangaung, Mei mwaka jana.

Wawili hao wamekuwa mafichoni tangu picha zao kusambaa wakiwa wanafanya shopping J’burg, mapema mwaka huu.

Walinaswa mjini Arusha siku ya Jumatano iliyopita wakiwa na passport nyingi zenye majina tofauti tofauti.

Ingawa bado hajafunguliwa mashtaka rasmi, kulingana na polisi, atakabiliwa na mashtaka ya kusaidia na kusaidia kutoroka gerezani, mauaji, na udanganyifu.

Wakati akifikishwa mahakamani, Dk Nandipha aliunganishwa na baba yake mzazi, na wengine wanne akiwemo mfanyakazi aliyepewa kandarasi ya kufunga kamera za CCTV jela aliyokuwepo Bester.

Kesi dhidi ya Nandipha imeahirishwa hadi Aprili 17, 2023, na haijajulikana kama daktari huyo amebadilisha maelezo yake ya awali.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: