Menu ›
Habari
Wed, 16 Oct 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kiungo mshambuliaji wa Fountain Gate FC, Suleiman Mwalimu Abdallah ‘Gomez’ amechaguliwa mchezaji Bora wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara kwa mwezi Septemba, mwaka huu.
Aidha, Kocha wa Fountain Gate Mohamed Muya ameshinda Tuzo ya Kocha Bora wa mwezi Septemba Ligi Kuu, akiwapiku Mmorocco Rachid Toussi wa Azam FC na mzawa mwenzake, Dennis Kitambi wa Singida Black Stars.
Kwa upande wake, Suleiman Mwalimu Abdallah ‘Gomez’ ameshinda Tuzo hiyo dhidi ya William Edgar anayecheza naye Fountain Gate na Feisal Salum wa Azam FC.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: