Mwanamke mmoja mkazi wa Magomeni Mikumi jijini Dar es Salaam, amemuomba Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Dkt. Dorothy Gwajima pamoja na serikali kwa ujumla kumsaidia kupata haki ya mtoto wake wa kike wa miaka 7, aliyelawitiwa na mwanaume wa miaka 38, ambaye alikiri kutenda kosa lakini baada ya hukumu kutoka ameachiliwa huru na Mahakama ya Kinondoni.
Mwanamke mmoja mkazi wa Magomeni Mikumi jijini Dar es Salaam, amemuomba Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Dkt. Dorothy Gwajima pamoja na serikali kwa ujumla kumsaidia kupata haki ya mtoto wake wa kike wa miaka 7, aliyelawitiwa na mwanaume wa miaka 38, ambaye alikiri kutenda kosa lakini baada ya hukumu kutoka ameachiliwa huru na Mahakama ya Kinondoni. Anasema mara tu ya kugundua mtoto wake kafanyiwa ukatili huo alipomuuliza alimtaja huyo mwanaume na alipomfuata kumuuliza alikiri kutekeleza tukio hilo la kikatili na hata alipofika Polisi alikiri kutekeleza tukio hilo lakini aliomba asamehewe kutokana alitenda kwa kutotarajia, lakini ameshangaa Mahakama imemuachia huru mwanaume huyo.