Sun, 7 Jul 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Simba imethibitisha kumsajili beki wa kushoto Valentin Nouma kutoka klabu ya St. Eloi Lupopo ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwa mkataba wa miaka mitatu.
Nouma (24) raia wa Burkina Faso ana uwezo mkubwa wa kukaba na kushambulia kwa wakati mmoja lakini pia ni mtaalamu wa mipira iliyokufa.
Nouma anatarajiwa kusaidiana na beki wa kushoto na nahodha wa Simba Sc, Mohammed Hussein, Zimbwe Jr kwenye nafasi hiyo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: