Mon, 31 Jan 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Timu ya Taifa ya Senegal imefanikiwa kwenda Nusu Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika baada ya ushindi wa 3-1 dhidi ya Equatorial Guinea mchezo uliopigwa jana Jumapili katika Uwanja wa Ahmadou Ahidjo Jijini Yaoundé, Cameroon.
Mabao ya Simba wa Teranga yamefungwa na Famara Diedhiou dakika ya 28, akimalizia pasi ya Sadio Mane, Cheikhou Kouyate dakika ya 68 na Ismaila Sarr dakika ya 79, wakati la Equatorial Guinea limefungwa na Jannick Buyla dakika ya 57.
Senegal itakutana na Burkina Faso wakati Egypt itakutana wenyeji Cameroon katika michezo ya nusu fainali.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: