Nahodha wa Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Mbwana Ally Samatta amesema kuwa kilichowapeleka nchini Ivory Coast ni kushinda michuano ya AFCON na si vinginevyo. Samatta amesema hayo jana wakati akizungumza kwenye Mkutano na Waandishi wa Habari kuelekea mchezo dhidi ya Morocco utakaochezwa leo katika Dimba la Stade Laurent Pokou, Ivory Coast.
“Morocco ni timu kubwa na ngumu, ni moja ya timu bora sana kwa sasa Afrika na Duniani, hivyo tunawaheshimu lakini hilo halituzuii sisi kwenda kuoambana nao. Jambo moja lililotuleta huku ni Tanzania kushinda hii michuano,” amesema Samatta.
Wangapi wanaamini leo Taifa Stars itashinda mbele ya Morocco?