Tue, 25 Jan 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Magoli ya Sadio Mane dakika ya 63 na Bambia Dieng aliengia akitokea benchi kuchukua nafasi ya Sadio Mane aliefunga goli la pili dakika ya 90+2, yalitosha kuivusha Senegal hatua ya Robo Fainali michuano ya AFCON.
Katika mchezo huo uliwashuhudia Cape Verde wakimaliza watu tisa uwanjani baada ya wachezaji wake wawili kuonyeshwa kadi nyekundu.
P. Andrade na golikipa Vozinha walionyeshwa kadi nyekundu na kuwafanya Cape Verde kucheza pungufu dakika nyingi za mchezo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: