Klabu ya Real Sociedad imefuta uteja wa kushindwa kupata ushindi katika dimba la nyumbani la Barcelona (Nou Camp) kwa mara ya kwanza tangu 1991 ikiwa ni msururu wa mechi 24 bila ushindi katika dimba hilo na kufufua matumaini ya kumaliza katika nafasi nne za juu kwenye msimamo wa Ligi kuu Uhispania.
Katika mchezo huo wa Ligi Kuu ya Hispania (La Liga) barcelona walikubali kichapo cha magoli 2-1.
Mabao ya Sociedad yamewekwa wavuni na Merino 5', Sorloth 72' huku bao la Barcelona likifungwa na Lewandowski dakika ya 90.
wa ushindi huo Real Sociedad imetibua sherehe za Barcelona za ubingwa wa Laliga ambao wamepokea kichapo cha kwanza nyumbani msimu huu katika siku ambayo wamekabidhiwa ubingwa wa LaLiga.