Wekundu wa Msimbazi Simba SC wanashuka Dimbani muda mchache kutoka sasa kuwakabili Maafande wa Tanzania Prisons katika Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya.
Mchezo huo wa mzunguko wa nne wa Ligi Kuu Tanzania Bara unawashuhudia Simba wakihitaji alama tatu kwa kila hali ili kupata nafasi ya kwenda kushikilia msimamo wa Ligi Kuu Bara wbaada ya wenzao Azam FC kulazimishwa sare na Dodoma Jiji huku Yanga wakipokea kichapo cha mabao 2-1 dhidi ya Ihefu.
Simba watahitaji kutengeneza wigo wa alama ili kujiweka katika mazingira mazuri ya kubeba ubingwa mwishoni mwa msimu.
Hiki hapa kikosi cha Simba kinachokwenda kuanza mchezo wa leo;