Mon, 22 Jan 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Bao la kuongoza la Taifa Stars dhidi ya Zambia katika dakika ya 12, limemfanya Simon Msuva afikie idadi ya mabao 23 yaliyofungwa na nahodha wake Mbwana Samatta katika mechi tofauti za kimashindano za timu hiyo.
Lakini pia limemfanya Msuva abakishe mabao mawili tu ili aifikie rekodi ya Mrisho Ngassa ya kuwa mfungaji bora wa muda wote wa Taifa Stars akiwa na mabao 25.
Kabla ya kufunga bao hilo la kwanza, Msuva alikuwa nafasi ya tatu katika chati ya wafungaji bora wa muda wote wa Taifa Stars, nyuma ya Ngassa na Samatta.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: