Mpinzani wa Simba Ligi ya Mabingwa Afrika, Wydad Casablanca inaendelea kucheza mechi za Ligi Kuu ya nchini Morocco amabapo kesho Desemba inaikari-bisha Mouloudia Oujda kabla ya kukutana na Simba Desemba 9 Uwanja wa Mohamed V nchini humo.
Simba inapaa leo usiku kwenda nchini Morocco, itakiwasha na Wydad AC Jumamosi saa 4:00 usiku.
Hata hivyo safari hiyo ya zaidi ya masaa matano ambayo itailazimu Simba kupanda ndege mbili hadi tatu tofauti ni ya kimkakati zaidi ambapo kocha mkuu mpya wa kikosi hicho, Mualgeria Abdelhak Benchikha ndiye amependekeza timu kuwahi ili ijiandae na walau kwa siku mbili.