Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Michezo mitatu Ligi Kuu kupigwa leo

Yanga 6 WA0005 Michezo mitatu Ligi Kuu kupigwa leo

Thu, 29 Aug 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Bingwa wa Kombe la Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga leo inaanza kampeni ya kutetea taji hilo ugenini dhidi ya Kagera Sugar.

Mchezo huo utafanyika kwenye uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba.

Katika mchezo wa mwisho wa Ligi Kuu timu hizo kukutana Mei 8 mwaka huu kwenye uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam Yanga ilishinda kwa bao 1-0.

Mchezo mwingine wa Ligi Kuu leo KMC itakuwa wenyeji Coastal Union kwenye uwanja wa KMC Complex, Kinondoni Dar es Salaam.

KMC na Coastal Union zilitoka suluhu katika mchezo wa mwisho wa Ligi kati ya timu hizo Mei 28 mwaka huu.

Kwenye uwanja wa Majaliwa, Lindi wenyeji Namungo itaikaribisha Fountain Gate.

Yanga, Coastal Union na Azam ambayo imecheza Agosti 28 dhidi ya JKT Tanzania zimechelewa kuanza ligi kutokana na majukumu ya kimataifa.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: