Crescentius Magori ambaye ni Mshauri wa Rais wa heshima wa Simba Bw.Mohammed Dewji, amesema kuelekea mechi yao ya marudiano hapo kesho dhidi ya Al Ahly huko Misri basi wachezaji wao inabidi wajitoe ili kuupata ushindi maana hiyo ni timu ngumu sana ikiwa kwao.
Crescentius Magori ambaye ni Mshauri wa Rais wa heshima wa Simba Bw.Mohammed Dewji, amesema kuelekea mechi yao ya marudiano hapo kesho dhidi ya Al Ahly huko Misri basi wachezaji wao inabidi wajitoe ili kuupata ushindi maana hiyo ni timu ngumu sana ikiwa kwao. "Simba tuna wakati mgumu sana katika mchezo na Al Ahly wa marudio na wala tusidanganyane,inabidi wachezaji wakafanye kazi zaidi na kujitolea,ingawa hakuna kinachoshindikana kwani mwaka 2003 tuliwatoa mabingwa Zamaleki enzi hizo huko huko kwao kipindi ambacho wengi hapa Tanzania walikua wametukatia tamaa" amesema Magori