Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa zamani wa Simba aliyewahi kuhudumu pia katika nafasi ya Katibu Mkuu Mwina, Yusuf Kaduguda anabainisha kwamba tangu kuanzishwa kwa Simba, Murtaza Mangungu ndio amekuwa mwenyekiti wa kwanza wa Simba akiwa madarakani timu imepoteza mechi tatu mfululizo dhidi ya Yanga.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa zamani wa Simba aliyewahi kuhudumu pia katika nafasi ya Katibu Mkuu Mwina, Yusuf Kaduguda anabainisha kwamba tangu kuanzishwa kwa Simba, Murtaza Mangungu ndio amekuwa mwenyekiti wa kwanza wa Simba akiwa madarakani timu imepoteza mechi tatu mfululizo dhidi ya Yanga. “Kuna timu zote duniani unaweza kucheza navyo utakavyo, lakini kuna Yanga ya kucheza na Yanga ni kitu kingine kabisa, mdogo wangu Mangungu amekuwa na bahati mbaya sana, ndio maana nasisitiza kucheza na Yanga hiyo ni mechi nyingine kabisa,” amesema Mwina Seif Kaduguda ‘Simba wa Yuda’.