Sat, 10 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Michuano ya kombe la Mataifa Afrika inaendelea tena leo Februari 10, 2024 kwa mechi moja ya kuwania nafasi ya mshindi wa tatu kati ya Afrika Kusini vs DR Congo.
Mchezo huo utapigwa saa tano usiku katika uwanja wa Félix Houphouët-Boigny, Abidjan.
Timu hizi ziliondoshwa katika hatua ya nusu fainali, Bafana Bafana wakitupwa nje kwa mikwaju ya penalti 4-2 dhidi ya Nigeria kufuatia sare ya 1-1.
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ilisukumizwa nje kufuatia kipigo cha 1-0 dhidi wenyeji, Ivory Coast.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: