Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

CAF Kufuta Mashindano ya AFCON Mwezi Ujao?

CAF Afcon CAF Yakanusha Uvumi Kuhusu Kufuta AFCON

Thu, 9 Dec 2021 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Shirikisho la Mpira wa Miguu barani Afrika (Caf), limekanusha uvumi kwamba Kombe la Mataifa ya Afrika (Afcon) mwezi ujao linaweza kuondolewa kutoka Cameroon kufuatia ugunduzi wa hivi majuzi wa aina mpya ya Omicron ya Covid-19.

Aina hiyo mpya ya virusi vya corona imesababisha vikwazo vya usafiri kuanzishwa na baadhi ya nchi kwa mataifa kadhaa ya Afrika, huku Nigeria, ambayo jirani na Cameroon, ndiyo ya hivi punde zaidi kuongezwa kwenye ‘orodha nyekundu’ ya Uingereza.

Katika siku za hivi karibuni, baadhi ya mashirika ya vyombo vya habari yamependekeza tarehe za mchuano huo wa timu 24 zinaweza kubadilika au hata eneo kuhamishwa,na kupelekwa Qatar.

Mkurugenzi wa mawasiliano wa Caf Alex Siewe anasema sio shirikisho wala maafisa wakuu wa Cameroon ambao wamejadili matukio kama hayo. “Hatuwezi kuendelea kutumia muda kushughulika na uvumi,” aliambia BBC Sport Africa.

“Hatukupokea ujumbe au taarifa nyingine yoyote kutoka kwa viongozi wetu – hakuna kitu kama hicho cha kubadilisha tarehe au nchi. Hatukujadili mambo kama hayo wakati wa mikutano yetu yote iliyopita.”

“Tuko kwenye tovuti. Tunafanya kazi.” Michuano ya barani Afrika, ambayo tayari yamecheleweshwa kwa sababu ya janga la corona, yanatarajiwa kuanza Januari 9 huko Yaounde na kumalizika mnamo 6 Februari.

Wafanyakazi wa Caf waliwasili Cameroon wiki hii kuandaa fainali za Afcon. “Ujumbe rasmi kutoka Caf umetolewa na katibu mkuu Veron Mosengo-Omba anajiunga nasi baada ya siku mbili,” aliongeza.

Chama cha Vilabu vya Ulaya, chombo huru kinachowakilisha vilabu Ulaya, kimeelezea “wasiwasi wake mkubwa” kuhusu ustawi wa wachezaji kabla ya mashindano, na kuongeza kuwa hali ya afya ya umma “inaendelea kuzorota kwa njia ya kutisha”.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: