Mon, 17 Jan 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kikosi cha Timu ya Taifa ya Algeria kimekubali kichapo cha bao 1-0 kutoka kwa Equatorial Guinea.
Kipigo hicho walichokipata Algeria kinamaliza rekodi yao ya kucheza michezo 35 pasipo kupoteza.
Kipigo hicho kinaweka rehani nafasi ya kufuzu kwa hatua inayofuata kwa mabingwa hao watetezi wa AFCON kwani mpaka sasa wana alama moja tu wakishika mkia katika kundi E.
Ugumu kwa Algeria ni kuwa wanahitajika kuwafunga Ivory Coast katika mchezo wa mwisho wa hatua ya makundi.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: