Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Barcelona yamsajili Mikayil wa Senegal

Mikayil E.jpeg Barcelona yamsajili Mikayil wa Senegal

Mon, 19 Jun 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Barcelona imethibitisha kumsajili Mikayil Faye kwa ajili ya msimu ujao, mchezaji wa Senegal aliyeichezea NK Kustosija Zagreb na ambaye amesajiliwa kwa misimu minne ijayo, hadi 2027 .

Beki huyo atakuwa na kipengele cha kumnunua cha euro milioni 400.

Beki huyo wa kati anasimama vyema kwa nguvu zake za kimwili na udhibiti mzuri wa mpira kutoka upande wa kushoto wa ulinzi, mchezaji mwenye kasi na akili yake uwanjani tayari imemruhusu kuwa mchezaji wa kimataifa na timu ya U17 ya Senegal.

Faye, 18, amekubali mkataba na klabu hiyo ya Catalan hadi 2027 na kifungu chake cha kuachiliwa kimepangwa kuwa €400m.



Barca haijathibitisha ada hiyo, lakini vyanzo vinasema gharama ya awali ya uhamisho huo, kabla ya kujumuisha nyongeza zinazowezekana, ni karibu €1.5m.

Faye atakuwa sehemu ya kikosi cha Rafa Marquez, Barca Atletic, ambacho kinashiriki ligi daraja la tatu la soka la Uhispania.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: