Mastaa Yanga, Stephanie Azizi na Djigui Diarra leo Septemba 08 watashuka uwanjani katika michezo ya mwisho hatua ya makundi kufuzu Afcon 2023.
Azizi Ki ataiwakilisha Burkina Faso katika Uwanja wa Stade de Marrakech dhidi ya Eswatini huku Diara akiwa nyumbani, Uwanja Stade du 26 Mars Mali ikiialika Sudan ya Kusini.
Burkina Faso ni kinara wa kundi B ikiwa na pointi 10 ikifuatiwa na Cape Verde 10, Togo ya tatu na pointi 5 na Eswatini akihitimisha kundi na pointi 2.
Mali inaongoza kundi G ikiwa na pointi 12 ikifuatiwa na Gambia yenye 9 ikitofautiana pointi tatu na Congo huku Sudani ya Kusini inashika mkia na pointi 3.