Mon, 4 Sep 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kocha Mkuu wa kikosi cha timu ya taifa, Algeria Djamel Delmadi amemjumuisha kiungo mkongwe Sofiane Feghouli (33) katika kikosi chake kwa ajili ya mchezo wa kutafuta nafasi ya kufuzu AFCON dhidi ya Tanzania, September 7.
Sofiane ambaye ni kiungo mshambuliaji amerudi kikosini humo kwa mara ya kwanza baada ya kukosekana kwa mwaka mmoja.
Mara ya mwisho Sofiane kuitwa kikosini humo ilikuwa ni kwenye mchezo wa mtoano kufuzu Kombe la Dunia 2022 dhidi ya Cameroon ambao walipoteza.
Sofiane alikuwa sehemu ya kikosi cha Algeria kilichopata ushindi wa mabao 7-0 dhidi ya Taifa Stars mwaka 2018.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: