Fri, 28 Apr 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kwa mujibu wa mtandao wa Goal, miamba ya Soka Barani Afrika, Al Ahly ya Misri wameingia kwenye kinyang'anyiro cha kumsajili mshambuliaji kinara wa Marumo Gallants, Ranga Chivaviro.
Chivaviro ambaye ni raia wa Afrika Kusini ni miongoni mwa wafungaji bora wa michuano ya Kombe la Shirikisho la CAF akiwa na mabao 5 sawa na Fiston Kalala Mayele.
Al Ahly sio timu pekee kwenye mbio hizi kuna timu kama Zamalek, Young Africans na Orlando Pirates wote wanatajwa kuitaka huduma ya Chivaviro.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: