Sun, 23 Jan 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Timu ya taifa ya Burkina Faso imekuwa timu ya kwanza kutinga hatua ya robo fainali ya AFCON kwa kuiondosha timu ya taifa ya Gabon kwa changamoto ya mikwaju ya penati 7-6 Baada ya timu hizo kumaliza dakika 120 kwa sare ya kufungana 1-1
Gabon licha ya kucheza pungufu kwa muda mwingi wa mchezo huo, wameonesha ushindani mkubwa na kutoa tafsiri nyingine ya ugumu wa michuano hiyo inayoendelea huko Cameroon.
Zimepigwa jumla ya penati 9, Gabon wamekosa 3 na Burkina Faso wakakosa 2. Burkina Faso katika robo fainali watakutana na Tunisia ambaye naye amemfunga Nigeria kwa bao 1-0.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: