Fri, 18 Feb 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na wenzake watatu wataanza kujitetea Machi 4, 2022 katika kesi ya ugaidi inayowakabili.
Hiyo ni baada ya Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi kuwakuta na kesi ya kujibu.
Leo Ijumaa Februari 18, 2022 Mbowe na washtakiwa wenzake ambao ni Halfan Bwire Hassan, Adamu Hassan Kasekwa maarufu kama Adamoo na Mohamed Abdillahi Ling’wenya wamekutwa na kesi ya kujibu
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: