Kiongozi wa jopo la utetezi katika kesi ya ugaidi inayomkabili Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na wenzake watatu, Wakili Peter Kibatala leo Jumatatu Januari 31,2022 ameendelea kumhoji shahidi wa 12 wa upande wa mashtaka ikiwa ni siku ya tatu mfululizo shahidi huyo kuhojiwa na upande wa utetezi huku mahojiano yakitarajiwa kuendelea kesho.
Shahidi huyo, Luteni Denis Urio wa upande wa mashtaka ameendelea kuhojiwa na Kibatala katika hatua ya udodosaji.
Mchuano baina ya Luteni Urio na mawakili wa utetezi ulianza Alhamisi, baada ya kumaliza kutoa ushahidi wake wa msingi aliouanza Jumatano ya wiki iliyopita huku akiongozwa na mwendesha mashtaka, Wakili wa Serikali Mwandamizi, Abdallah Chavula katika Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi.
Leo Jumatatu Kibatala aliendelea kumhoji Luteni Urio kuanzia asubuhi mpaka jioni Jaji Joachim Tiganga alipoahirisha kesi hiyo mpaka kesho Jumanne ambapo Kibatala ataendelea kumhoji shahidi huyo.
Kabla ya Jaji Tiganga kuahirisha kesi hiyo, Kibatala alitoa hoja ya kuomba kesi iahirishe mpaka kesho akidai kuwa bado ana maswali mengi, hoja ambayo iliunga mkono na upande wa mashtaka.
Ifuatayo ni mahojiano baina ya wakili wa utetezi Peter Kibatala na shahidi Luteni Urio
Jaji Joachim Tiganga ameingia mahakamani na kesi inatajwa na karani
Kiongozi wa jopo la Waendesha mashtaka Wakili wa Serikali Mwandamizi, Robert Kidando anafanya utambulisho.
Sasa kiongozi wa jopo la mawakili wa utetezi, Peter Kibatala anafanya utambulisho wa jopo lake.
Jaji Tiganga anawaita washtakiwa kwa kutaja namba zao kwenye kesi kuanzianza kwanza hadi wa nne na wote wanaitika.
Wakili Kidando: Shauri linakuja kwa ajili ya kuendelea kusikilizwa na Shahidi wetu yupo.
Wakili Kibatala: Nasi Mheshimiwa Jaji tuko tayari
Sasa Wakili Kibatala anaanza kumhoji shahidi. Shahidi huyo, Luteni Denis Urio wa upande wa mashtaka.
Wakili: Mhe Urio good morning
Shahidi: Morning too
Wakili: Naendelea kukuuliza maswali. Ukiacha tukio hili umewaji kukutana na tikio longine kubwa la kigaidi kama hili?
Shahidi: Hebu rudia
Wakili: Ulishawahi kukutana na mtu mnayefahamiana akakwambia matukio mazoti kama haya au ni mara yako ya kwanza?
Shahidi: Ni sahihi
Wakili: Ulisama huna matatizo ya kumbukumbu?
Shahidi: Sahihi
Wakili: Sasa Shahidi inawezekana vipi ukasahau tarehe muhimu kama hizi za tarehe ya kukutana na Mbowe kukwambia masuala haya na tarehe ya kwenda kwa DCI na hasa Askari mkubwa kama wewe mwenye cheo cha Luteni?
Shahidi: Ni mara ya kwanza kupata taatifa kama hizo kwa Mheshimiwa Mbowe hivyo sikuamini mara moja lakini angekuwa na rekodi kama hizo ningejua.
Wakili: Vipi kukumbuka kwenda kwa DCI?
Shahidi: Sijakumbuka kwa sababu si duty yangu ya kufanya uchunguzi.
Wakili: Sawa, unaweza kusaidia kwa nini hata DCI katika maelezo yake hakumbuki?
Shahidi: Siwezo kumjibia DCI
Wakili: Unafahamau au hufahamu?
Shahidi: Sifahamu
Wakili: Je kwa nini hata ACP Kingao ambaye alikuwepo naye hafahamu?
Shahidi: Sijui kwa nini hajui
Wakili: Na kuhusu ofisa mwingine wa Polisi, Afande Swila naye hafahamu?
Shahidi: Sifahamu
Wakili: Wewe unaona hii hali ni ya kawaida?
Shahidi: Nilikwenda ofisi ya mtu sasa siwezi kumlazimisha kutake note.
Wakili: Unafahamu kwa nini maelezo yako yaliandikwa karibu mwezi mmoja baadaye badala ya kuwa ya kwanza?
Shahidi: Sifahamu
Wakili: Huoni kwamba ni busara maeelezo ya mtu muhimu kama wewe mtoa taarifa kuandikwa mapema?
Shahidi: Sielewi utaratibu wake yeye kama anaona inafaa
Wakili: DCI alikufafanulia kwa nini maelezo yako hayakuchukuliwa mapema?
Shahidi: Hawakunifafanulia
Wakili: Tarehe 11/8/2020 ndio ulikwenda kwa Inspekta Swila kuandika maelezo yako ya tukio zito la kupanga njama na makomandoo, Swila alikufafanulia?
Shahidi: Hakunifafanulia
Wakili: Tukiamini kwamba tuhuma zilitungwa kwanza ndipo wakatafutwa washtakiwa tunakuwa tunakosea?
Shahidi: Utakuwa unakosea.
Wakili: Katika kikao chenu wewe DCI na Kingao mliwahi jadili mbinu ya kumtuma Askari wa Polisi aende kwa Mbowe ajifanye ili kupata ushahidi kwa sababu wao wako trainees na wana vifaa?
Shahidi: Mimi sikuwahi kujadili
Wakili: Ni kweli kwamba katika ushahidi wako kuwa Mbowe alisema anataka kuchukua dola kwa namna yoyote na gharama yoyote kwenye uchaguz wa 2020
Shahidi: Ni kweli
Wakili: Na Bado unasisisitiza kwamba kwa hizo factor wewe hukuwa ni mwanajeshi kazini na wanaotakiwa Ni X Commandos bado jeshi halikujitaji kuchukua hatua?
Shahidi: Kwa sabau ni taarifa zilizotolewa kwenye uraia kwa hiyo bado zingerudi polisi maana ni taarifa ambazo hazikuwa sahihi.
Wakili: Unamfahamu aliyekuwa Luten Shimbo?
Shahidi: Namfahamu
Wakili: Kwamba Oktoba 13, 2010 Luten Shombo alisema kuwa uchaguzi unakuwa wa amani na kwamba Jeshi liko tayari kuchukua nchi kama kungetokea uvunjifu wa amani
Shahidi: Sikuwahi kusikia
Wakili: Kwa nini Hamkuona kwa taarifa hizo ambazo zinawahusisha makomandoo mngetuma makomandoo kuwa kama mamluki?
Shahidi: Kwanza Mbowe alikuwa hapokei simu na aliomba picha zao ili afanya research kama wako kazini.
Wakili: Kwa hiyo Freeman Mbowe ana mbinu za kufanya cross checking za Askari?
Shahidi: Ndio, kwa nini alitaka picha zao, kwa nini alitaka kujua umri wao
Wakili: Katika ushahidi wako ulisema Mbowe ana access na mtu mwingine jeshini?
Shahidi: Sikusema
Wakili: Kwa hiyo ni kweli kwamba kuna mambo ulikuwa huyafahamu hujui kama Mbowe alikuwa na plan A na B?
Shahidi: Ndio
Wakili: Unasema hukuwa na uhakika kama Mbowe alikuwa na plan A na B na Mbowe alikuwa na trust na wewe ulimhoji kama alikuwa na mtu mwingine ambaye alikuwa ameshamu-approach?
Shahidi: Sikumhoji
Wakili: Kwa assessment yako alikuwa anakuamini?
Shahidi: kuwa alikuwa ananiamini Mimi peke yangu?
Wakili: Na unasema alikuahidi cheo Kikubwa jeshini kama?
Shahidi: Kwa mawazo yake yeto, Mbowe hawezi kunipa cheo
Wakili: Baada ya kuachana na Mbowe mawazoni mwako ulikuwa umeshamkubalia au kumkatalia?
Shahidi: Kumkatalia
Wakili: Na kweli wakati anakwambia ulikuwa unamsikiliza tu na kwawmba ngoja amalize tu nakwenda kutoa taarifa?
Shahidi: Kuna hatua…
Wakili: Akili ya kawaida ya Luteni haikuweza kum-probe ili iujua huyu anapanga kulipua vituo vya mafuta au ni viongozi gani?
Shahidi: Kwa akili ya kawaida hata kama ni wewe ukishaanza kumdodosa anastuka.
Wakili: Utakubaliana na Mimi kwamba neno lako wewe dhidi ya neno la Mbowe na hakuna ushahidi wa sauti wala hamkutuma decoy?
Shahidi: Ndio maana tulituma hao vijana
Wakill: Hawa Ni washtakiwa kwani hawa ni mashshidi wenu?
Shahidi: Waliiingia kwenye uhalifu wenyewe
Shahidi: Unakumbuka lini uliongea na Ling'wenya?
Shahidi: Sikumbuki
Wakili: Ni kweli kwamba mzee Ling'wenya alikuwa aataka umwachia mwanaye kuhusu hiyo kazi kutokana na historia ya yale yaliyotokea jeshini?
Shahidi: Sifahamu
Wakili: Una ugomvi na mzee Ling'wenya mpaka akutungie hayo?
Shahidi: Sitahamu na wala sijawahi kumuona
Wakili: Unatajambua kuwa mzee Ling'wenya moyo wake unavuja damu kwa haya anayopitia kwa mwanaye uliyemuomba kuwa unamtafutia kazi ?
Shahidi: Sifahamu, kwani mwanaye aliambiwa kwamba akashiriki uhalifu?
Wakili: Alipokuuliza kuhusu mwanaye kukamatwa ulimpa ushirikiano gani?
Shahidi: Nilimwambia aongee na bosi wake.
Wakili: Ulimweleza mzee Ling'wenya ukweli kwamba Mbowe ana mipango ya ugaidi kwa hiyo tunataka kumtumia mwanao ili kupata ushahidi?
Shahidi: Sikumwambia
Wakili: Umeshawahi kusikia neno kumtoa mtu kafara?
Shahidi: Nafahamu
Wakili: Siku ya kwanza nilikuuliza maswali mengi kuhusu kwenda kanisani ukasema wewe ni Mkristo, Unamfahamu Daniel kwenye Biblia?
Shahidi: Namfahamu
Wakili: Unafahamu walichomfanyia?
Shahidi: Nafahamu walimtupa kwenywe tundu la Simba
Wakili: Unafahamu kwanza walimuingiza kwenye mtego kwa kumwambia atunge sheria, Mkristo mwenzangu huoni kuwa hicho ulichomfanyia mzee Ling'wenya kinafafana na hicho alichofanyowa Daniel?
Shahidi: Ni tofauti kabisa
Wakili: Na Mkristo mwenzangu moyo wako uko sawa tu?
Shahidi: Sawa kabisa
Wakili: Unafajamu mzee Ling'wenya ametumikia nchi hi bila doa?
Shahidi: Sifahamu
Wakili: Ni mazingira gani kiongozi anaweza kuondoka na kuwaacha askari wake
Shahidi. Huwezi kukaa sehemu moja na wafuasi wako wafuasi wanatakiwa kukaa mbele na kiongozi nyuma
Wakili. Unafahamu Adam Kasekwa aliachishwa kazi kwa kupata tatizo la kisaikolojia
Shahidi. Hana historia hiyo
Wakili. Kwenye maelezo mliyoleta mnasema ana historia hiyo
Shahidi. Kwani ameleta cheti cha daktari
Wakili. Ulifahamu sababu mahususi ya Ling'wenya kuachishwa kazi
Shahidi. Kwa utovu wa nidhamu
Wakili. Kwa kuwa uliwasiliana na Bwire unafahamu ni maeneo gani mahususi walitembelea kwaajili ya kumdhuru Sabaya
Shahidi. Bwire hakuniambia
Wakili: Unafahamu allegation ilikuwa ni kumdhuru Sabaya kwenye maeneo hayo
Shahidi: Aliieleza in breif lakini hakuniambia ni maeneo gani
Wakili. Nani aliyetumwa kumtafuta Mbowe ni nani
Shahidi. Ni mimi
Wakili. Mbowe aliomba polisi wamtafutie vijana
Shahidi: Hakuomba
Wakili: Ni kweli uliandika maneno hayo katika maelezo yako
Shahidi: Ni kweli
Wakili: Polis walikuwa na mawasiliano na Bwire
Shahidi; Hawakuwa nayo
Wakili: Nani alikuwa anaaminiwa na Bwire na Adamoo
Shahidi: Ni mimi
Wakili: Kuna msiri alikuwa anawapa wakina Kingai taarifa na kueleza walivyovaa ni wewe
Shahidi: Sio mimi
Wakili: Kingai aliwahi kukwambia kuna msiri wao mwingine zaidi yako
Shahidi: Hapana
Wakili: Kuna mtu mwingine alikuwa anawafahamu kadri waeleze walivyokuwa wamevaa
Shahidi: Sifahamu
Wakili: Unafahamu walichokuwa wanafanya pale Rau Madukani
Shahidi: Sifahamu
Wakili: Unafahamu Ling'wenya ana dada yake pale Rau madaukani walikuwa wameenda kumsalimia
Shahidi: Sifahamu
Wakili: Unafahamu Ling'wenya ana dada yake anaishi Sakina Arusha
Shahidi: Haikuwahi kuniambia
Wakili: Kati maelezo yako uliandika ulimpa Kingai namba za simu ili aweze kuwa fuatilia
Shahidi. Ni sahihi
Wakili. Wakati unaaongozwa na wakili uliongelea kuwa ulimpa Kingai namba za simu
Shahidi. Sikuongelea
Wakili. Ni muhimu au sio muhimu
Shahidi. Ni muhimu
Wakili. Unafahamu maana yake kuzungumzia suala la namba ya simu
Shahidi. Sifahamu
Wakili. Unafahamu nama ndugu walivyohangaika kuwatafuta ndugu zao kwenye vituo vya polisi na hospitali
Shahidi. Sifahamu
Wakili: 11/8/2020 uliandikishwa maelezo na kumkabidhi simu zako wakati Swilla anachukua simu yako alikuruhusu kutoa line
Shahidi. Ni sahihi
Wakili. Ulimwambia Jaji kuwa uliondoka na simu line yenye mawasiliano yako
Shahidi: Kulikuwa na line mbili
Wakili: Line ya Vodacom ulimwambia Jaji tarehe 12 uliirusha
Shahidi: Nilimwambia
Wakili: Hiyo nakala ya makabidhiano ya line ya voda ulikuja nayo
Shahidi: Sikujua kama itahitajika mahakamani
Wakili: Tukiomba tukague simu kama line ipo?
Shahidi. Vyovyote itakavyowezekana
Wakili. Mheshimiwa Jaji naomba kielelezo namba 34
Wakili Kibatala anampa Shahidi simu aiwashe ili wakague laini iliyopo.
Shahidi: Hakuna line hata moja
Wakili: Unajua maana ya kiapo chako
Shahidi: Nafahamu
Wakili: Unajua ukweli na uongo unapimwa kwa vitu vidogo vidogo kama hivi
Shahidi: Nafahamu
Wakili:Wakati unaamkabidhi Inspekta Swilla simu ilikuwa na line
Shahidi: Ndio ya Airtel
Wakili: Iko wapi
Shahidi: Sifahamu
Wakili: Ushahidi wako wa mdomo ulimkabidhi Swilla simu tatu utaungwa mkono na nini
Shahidi: Kwa sababu ziko hapa
Wakili: Unafahamu simu hizi tatu ni za muhimu kwa kuwa zilikuwa na mawasiliano flani
Shahidi: Nafahamu
Wakili: Ulimwambia Jaji simu mbili ulizozifuata uliziacha kwa nani
Shahidi: Nilimwambia
Wakili: Ulimwambia uliziacha chini ya uangalizi wa nani
Shahidi: Sikumwambia
Wakili: Unafahamu ni kwanini kataika maelezo ya Inspekta Swilla hazungumzii simu tatu
Shahidi: Sihitaji kufahamu
Wakili: Unafahamu Freeman Mbowe alikuwa na kaka mwenye cheo kikubwa jeshini na Rais Magufuli alihudhuria Msiba huo
Shahidi: Nilisikia
Wakili: Unataka tuamini Mbowe alimuacha kaka yake wa damu akakutafuta wewe
Shahidi: Alishastaafu
Wakili: Wewe na General nani anafahamu watu wengi zaidi
Shahidi: Yeye
Wakili: Unasema ulishangaa mara ya kwanza Mbowe kukupiga simu
Shahidi: Ndio
Shahidi: Unafahamu mtu kuwa na mawasiliano yako unaweza kulalamika
Shahidi: Mimi sio mtu wa muhimu
Wakili: Unafahamu mtu kukusumbua unaweza kulalamika
Shahidi: Sifahamu
Wakili: Ulitoa taarifa
Shahidi: Sikutoa taarifa
Wakili: Katika maelezo yako uliandika ulikuwa na ukaribu na Mbowe kwa kuwa ni kabila moja
Shahidi: Ni sahihi
Wakili: Nini kilikupa comfort hadi ukaendelea kuwasiliana naye
Shahidi: Mbowe ni Mbowe na Chama ni Chama
Wakili: Katika maelezo yako ulitenganisha
Shahidi: Sikutenganisha
Wakili: Unasema ulitumiwa 500,000 ukatoa 300 000 ukabakiwa na 200,000
Shahidi: Ni sahihi
Wakili: Unakumbuka ulichoandika katika maelezo yako
Shahidi: Nakumbuka
Wakili: Katika maelezo yako umesema ulipopokea ulizitoa zote
Shahidi. Hapana sikuzitoa
Wakili. Unakubaliana na mimi ulitoa 300000 na 200000 zikabaki kwenye simu
Shahidi. Ni sahihi
Wakili. Uliambiwa maana ya haya maelezo
Shahidi: Sikuambiwa
Wakili: Hakuna mahali uliposema hii hela zote ulizitoa mfukoni
Shahidi: Ni sahihi
Wakili: Utakubaliana na mimi ulichokisema na kilichaoandikwa vinatofautiana
Shahidi. Ni sahihi
Wakili: Ulimwambia Jaji 40000 ilienda wapi?
Shahidi: Sikumwambia
Wakili: Katika maelezo yao wanasema uliwapa Sh 87, 000 kila mtu?
Shahidi: Sikumpa mmoja mmoja hela
Shahidi: Kwahiyo katika haya maelezo na unacho sema wewe ni tofauti
Shahidi: Ni tofauti
Wakili: Unakubali au unakataaa jumla ni Sh174, 000
Shahidi: Amount hiyo siwezi kuifahamu
Wakili: Ushahidi huu na wako unatofautiana?
Shahidi: Unatofautiana
Wakili: Fedha ulizotumiwa na Mbowe ilikuwa kuwagharamia nauli zao za kuja Morogoro
Shahidi: Ni sahihi
Wakili: Naomba nikusumbue tena Shahidi nisaidie kuwasha kielelezo namba 34 uende kwenye meseji ambazo ulizisoma
Shahidi: Tayari
Wakili: Ni kweli ulisema Mbowe alikuambia umtafutie makomandoo wasiokuwa na kikomo
Shahidi: Hakuniambia idadi
Wakili: 20/7/2020 meseji inasema idadi ni watatu au wanne
Wakili: Hebu isome kwanza
Shahidi: Kaka wale mtu tatu au nne ni muhimu siku zimeisha
Wakili: Hapa anataja mtu tatu au nne
Shahidi: Ni sahihi
Wakili: 20/7/2020 saa 2:3 hii meseji nani alituma
Shahidi: Mimi nilituma kwenda kwa Freeman Mbowe
Wakili: Hii ilituma kwa namba gani
Shahidi: Mtandao wa Telegram
Wakili: Ili iweze kusajili mtandao wa telegram si lazima uwe na simcard
Wakili: Ulitumiwa namba gani msomee Jaji asikie
Shahdi: 1130138344
Wakili: Imeandikwa owner Denis Urio
Wakili wa Serikali Mwandamizi Pius Hilla. Sio nia yetu kusimama Wakili kamwambia asome Shahidi kasoma lakini wakati anataka kutoa ufafanuzi Wakili hataki.
Wakili Kibatala: Mheshimiwa Jaji hiyo namba wameileta wao hawakutoa ufafanuzi anataka kufanya submission watatakiwa wamuulize Shahidi kwenye re examination
Jaji: Kama nimemsikia vizuri Kibatala anamuuliza Sahahid kama anaifahamu hiyo namba kabla ya kujibu akawa anataka kutolea ufafanuzi lakini kwenye cross examination shahidi anatakiwa kujibu kile anachoulizwa.
Wakili Kibatala: Hiyo namba unafahamu
Shahidi: Sifahamu
Wakili: Kuna mtu alikuongoza kufafanua hiyo namba
Shahidi: Hakuna
Wakili: Unafahamu application inaitwa Freeman sms
Shahidi: Sifahamu
Wakili: Kuna mtu alikuongoza au kukuuliza kama unafahamu free sms
Shahidi: Hakuna
Wakili: Simu yetu bado ina chaji
Shahidi: Ndio
Wakili: Kuna sehemu yoyote Mbowe anakwambia kutumia simu sio salama
Shahidi: Yah mwisho
Wakili: Isome
Shahidi: Hello bro nimeshindwa kupokea simu kwa sababu ya......
Wakili: Kwahiyo unataka kusema imefanana na hiyo usitumie simu sio salama sana
Wakili: Linganisha meseji uliyomsomea Jaji na hii hapa zimefanana?
Shahidi: Zinafanana
Wakili: some Jaji
Shahidi: 729414989
Wakili: Inasemekana ni ya nani
Shahidi: Free
Wakili: Zinafanana na za kielelezo ulichosaoma awali
Shahidi: Zinatofauti kubwa
Wakili: Tafuta sms ya tarehe 20/7/ 2020 ya saa 2:14 isome
Shahidi: Naomba nitumie nauli niwamobilize nikutane nao Morogoro
Wakili: Nani alikuwa anaomba nauli
Shahidi: Mimi
Wakili: Baada ya wewe kuomba nauli Mbowe ndio akatuma
Shahidi: Ni sahihi
Wakili: Nitafutie meseji ambayo Mbowe anatoa wazo la kutuma hiyo 500,000
Shahidi: Hakuna
Wakili. Ni nani kwa mujibu wa meseji aliyetoa wazo la kutuma 500,000
Shahidi: Ni mimi
Wakili: Kwa mujibu wa kielelezo namba 34 hiyo meseji ulituma kwa kutumia namba gani
Shahidi: Haionekani
Shahidi: Tafauta meseji ya tarehe 20 /7/2020
Shahidi: Nimeiona
Wakili: Usiwe unatumia namba yako kutuma pesa tumia Wakala au wasaidizi wako, Ni nani alituma ujumbe huu?
Shahidi: Ni mimi kwenda kwa Freeman Mbowe
Wakili: Hao wasaidizi waliwahi kukutumia pesa kutumia namba zao
Wakili: Unamfahamu msaidizi wa Mbowe anaitwa Wile
Shahidi: Sifahamu
Wakili: Kwenye mazungumzo yenu kwenye miamala ya kifedha hajawahi kuzungumzia mtu anaitwa Wile
Shahidi: Nimewahi
Mahakama imerejea baada ya mapumziko ya muda mfupi kwaajili ya Wakili wa utetezi Peter Kibatala kuendelea kumuhoji shahidi wa 12, Luten Denis Urio.
Mawakili wa pande zote wako tayari kuendelea
Wakili Kibatala: Mheshimiwa Jaji Naomba kielelezo namba 34 na 36
Wakili: Shahidi washa simu
Shahidi: Tayari
Wakili: Meseji ya tarehe 22/7/2020 saa 3:19:30 Namba ya dereva wangu anaitwa Wille atatuma pesa na ndio atawapokea ni sahihi
Shahidi: Ni sahihi
Wakili: Tarehe hiyo namba iliyotuma pesa iliingia kwenye simu yako
Shahidi: Ni sahihi
Wakili: Ni wapi unasema Freeman Mbowe alikutumia hiyo namba
Shahidi: Alituma kwa njia ya kawaida
Wakili: Iko wapi
Shahidi: Sikumbuki
Wakili: Huyu Wille hujawahi kukutana naye
Shahidi: Sijawahii kukutana naye
Wakili: Huyu Mbowe alikwambia umtafutie watu au magaidi
Shahidi: Kwaaji ya kwenda kuambatana naye na kufanya nchi isitawalike
Wakili: Kwahiyo wewe ulikuwa unamtafutia Mbowe watu kwaajili ya kufanya uhalifu
Shahidi: Walinzi
Wakili. Waliwahi kukwambia wakina Kingai unatakiwa uwe mshtakiwa namba moja au mbili
Shahidi. Hawakuwahi kuniaamba
Wakili: 22/7/2020 saa 12:27 hiyo sms nani alituma
Sahahid: Mimi kwenda kwa Freeman Mbowe
Wakili: Wakina Bwire walikuwa wameshaindoka kwenda kwa Mbowe
Shahidi: Ni sahihi
Wakili: Kwa maelezo haya inamaana ulitoa zote kwa pamoja
Shahidi: Ni sahihi
Wakili: Ushahidi wako na maelezo ni sahihi vinatofautiana au vinapishana
Shahidi: Vinaoana tofauti iko kwenye tafsiri
Wakili: Ulikuwa unashauri Mbowe awe anakutumia fedha za ziada
Shahidi: Ni sahihi
Wakili: Kwahiyo ulikuwa unamuomba ukijua anamipango ya kigaidi
Shahidi: Ni sahihi
Wakili: Ulishawahi kusikia neno soulitationi
Shahidi: Sijawahi
Wakili. Fedha hizi ulikuwa unaomba baada ya kupokea 500,000
Shahidi: Ni sahihi
Wakili: Ulisema kila hatua ulikuwa unamfahamisha Kingai
Shahidi: Ni sahihi
Wakili: Unaweza kutuonyesha meseji yoyote uliyomtumia Kingai
Shahidi: Hakuna
Wakili: Na meseji yoyote unayotumiwa fedha
Shahidi: Hakuna
Wakili: Kuna meseji inasomeka Shkamoo Mkuu
Shahidi: Ni sahihi
Wakili. Kwahiyo ulikuwa unamsalimia mtu anayeenda kutekeleza vitendo vya kigaidi
Shahidi. Ndio nilikuwa sina ugomvi naye
Wakili: Unasema Halfani Bwire alikupigia akakwambia wenzake wako Moshi wanaenda kutekeleza vitendo vya Kigaidi
Shahidi: Hakunipigia mimi ndio nilimpigia
Wakili: Katika maelezo yako uliandika kuwa wako Moshi wanampango wakumshambulia Sabaya
Shahidi: Mimi nilimpigia
Wakili. Unataka tuamini ulichokiandika Bwire naye yuko Moshi
Shahidi: Tumuulize
Wakili: Na katika maelezo yako uliandika Bwire yuko Dar es Salaam
Shahidi: Sikuandika
Wakili: Katika maelezo yako umeandika tukakutana tena na Freeman Mbowe limeingizwa kimakosa kwa sababu umesaini na kudthibitisha kuyasoma?
Shahidi: Sahihi
Wakili. Unasema kabla ya kukutana naye alikuwa anakutumia na ujumbe na kukutakia heri?
Sahahidi: Ni sahihi
Wakili: Mtu anayekutumia ujumbe na kukutakia heri ni mzalendo au sio mzalendo
Shahidi: Ni mzalendo
Wakili: Nani alikutafuta ni Freeman Mbowe au wewe ulimtafuta
Shahidi: Yeye ndio alinitafuta
Wakili: Kupitia nini
Shahidi: Simu na kupitia Whatsup call na namba nyingine
Wakili: Hizo namba ulizifikisha kwa DCI
Shahidi: Sikuzifikisha
Wakili: Nani aliandika maelezo yake kuwa nilimtafuta na kumwambia kuwa tunaweza kuonana.
Kuna sehemu umeandika kuwa ulimtafuta baada ya kukuita micdcall
Shahidi: Hamna
Wakili: Unaona kuna mfanano hapo au kuna tofauti
Shahidi: Kuna tofauti
Wakili: Kuna mahali ulipoandika kuwa baada ya kumpiga. DCI ulijutambulisha kama Ofisa wa jeshi
Shahidi: Nilijitambulisha
Wakili: Mheshimiwa Jaji kwa Ruhusa yako naomba wenzangu wanipe nyaraka halisi ya maelezo
Wakili: Maelezo ni ya kwako
Shahidi: Ni sahihi
Wakili: Nitafutie hiyo sehemu tafadhali
Shahidi: Hakuna
Wakili: Maelezo yako na ushahidi wako vinafana
Shahidi: Vinatofautiana
Wakili: Unakumbuka ulichojibu kwa wakili Mallya kuhusu kutumiana meseji
Wakili Kidando: Mheshimiwa Jaji naomba Shahidi asome maelezo yake kwanza
Wakili Kibatala: Mheshimiwa Jaji nyaraka hii inasomwa baada ya kuingia
Jaji: Utaratibu unasema nyaraka kwanza isomwe
Wakili Kibatala: Haya Shahidi soma maelezo yako.
Wakili: Ngerengere na Kihonda pana umbali gani
Shahidi: Kilomita 50 au 60
Wakil: Ulishamwambi Mheshimiwa Jaji unaishi Kihonda
Shahidi: Familia yangu iko kule
Wakil: Ulishawahi kusema hapa mahakamani kama kuwa unaishi Kihonda
Shahidi: Hapana
Wakili: Una matatizo na hayo maelezo
Shahidi: Hapana
Wakili: Unataka Jaji atende haki kabisa
Shahidi: Ndio
Wakili. Kuna tatizo tukiyatoa
Shahidi: Hakuna tatizo
Wakili. Mheshimiwa Jaji kama Shahidi alivyoomba
Jaji: Upande wa mashtaka mnasemaje
Wakili Kidando: Hatuna pingamizi Mheshimiwa
Jaji. Mahakama imepokea maelezo haya kama kielelezo namba nne cha upande wa utetezi.
Wakili: Shahidi simu bado ina chaji?
Shahidi: Ngoja niwashe
Wakili: Kuna meseji inasema kuwafanyia vetting ilikuwa vetting ya nini?
Shahidi: Kwa kuwa wanaenda kufanya kazi ya ugaidi ni muhimu kufanya vetting na wakiona vitendo vya kihalifu waniambie
Wakili: Hii meseji ulikuwa unajitumia mwenyewe au?
Shahidi: Nilikuwa natumia Freeman Mbowe
Wakili: Kuna kitu kingine cha ziada ulitaka kuwafanyia wakina Adamoo hadi ukaomba hela ya ziada kwa Mbowe.
Shahidi: Kwa kuwa hela ya awali ilishakuwa comshumd
Wakili: Ulikuwa unawafanyia orientation magaidi.
Shahidi: Ndio kwa fedha za Mbowe
Wakili: 22/7/2020 ulituma meseji inasema lakini wewe usitumie namba yako nani alituma
Shahidi: Mimi kwenda kwa Freeman Mbowe
Wakili: Kwa nini ulimtumia
Shahidi: Ili kuongeza Trust
Wakili: Nauli pamoja na hela za kula ni 2000, 000 nani alituma hiyo meseji
Shahidi: Mimi kwenda kwa Mbowe
Wakili: Hapa mlikuwa mnakubaliana nini kuhusu mishahara
Shahidi: Kwa hiyo kazi wanayoenda kuifanya
Wakili: Ni kazi gani hiyo
Shahidi: Ya uhalifu
Wakili: Kuna meseji inasema kuhusu utawala utawala ni nini
Shahidi: Chakula
Jaji: Nimepata taarifa kuna mafundi wanahitaji kufananya matengenezo tujitahidi angalau saa kumi na nusu tumalize.
Wakili Kibatala: Basi ngoja nisukumesukume hadi hapo kisha ntatoa hoja ya kuahirisha.
Wakili Piusi Hilla. Mheshimiwa Jaji tunaomba Wakili afanye cross kuna maeneo naona anarudia
Jaji. Ni vizuri unapouliza maswali ukatoa eneo hilo moja badala ya kurudia rudia.
Wakili Kibatala: Kama kuna sehemu anaona nimerudi au kama kuna swali basi aseme.
Wakili: Unaweza kufanya mlipuko bila kuwa na vya kulipiulia
Shahidi: Huwezi
Wakili: Katika ushahidi wako kuna sehemu ulisema bunduki aina ya luger ni mahusi kwaajili ya makomandoo kufanya ugaidi
Shahidi: Sijasema
Wakili. Baada ya Julai 24, 2020 uliwahi kuwasiliana tena na Mbowe
Shahidi: Nilikuwa nikimpigia hapokei nikamtumia meseji
Wakili: Ulikuwa unawasilia naye kwa meseji
Shahidi: Telegram
Wakili: Ulimuonyesha Jaji meseji ulizokuwa ukifanya juhudi za kumtafuta Mbowe
Sahahid: Sikufanya
Wakili: Tunakubaliana kilichoandikwa hapo ni simu yako na sio simu zako
Shahidi: Ni sahihi
Wakili: Uliongozwa na wakili wa Serikali kuonyesha rekodi zako za simu ulizokuwa unawasiliana na Bwire
Shahidi: Hapana
Wakili: Inspekta Swilla alikwambia na yeye ni mpelelezi kwenye shauri hili
Wakili: Sifahamu
Shahidi: Ni sahihi hukuwahi kusema kama uliandika maelezo ya ziada
Shahidi: Ndio
Wakili: Kambi ya makomandoo ipo Ngerengere au Kizuka
Shahidi: Kizuka
Wakili: Ulimwambia Jaji kuwa Kambi iko Kizuka na sio Ngerengere
Shahaidi: Ngerengere ni tarafa
Wakili Kibatala: Unakuambuka nilikwambia nini kuhusu namba DCI
Shahidi: Nakumbuka
Wakili: Ulisemaje
Shahidi: Nimeacha hotelini kwangu kwenye diary
Wakili: Ijumaa tulivyoachana hapa hadi leo na hujaja nayao
Shahidi: Nilisubiri nipewe maelekezo na mahakama
Wakili: Na wakili Mallya alikuuliza kuhusu Order nayo iko wapi
Shahidi: Hotelini kwangu
Wakili: Kwahiyo na leo nikihitaji haipo.
Wakili: Kipindi kinachohusiana na shauri hili ni kuanzia Juni 2020 hadi Agosti 2020
Shahidi: Ni sahihi
Wakili: Mbowe alikuwa anawasiliana na wewe kwa Telegram ili kuficha mawasiliano yenu
Shahidi: Ni sahihi
Wakili: Kabla ya tarehe hizo tukiangalia hatutakuta mahali mlikuwa mnawasiliana kwa telegram kabla ya tarehe hizo
Shahidi: Tulikuwa tunawasiliana kwa whatsup
Wakili. Ulimwambia Mheshimiwa Jaji wakati unamkabidhi Inspekta Swilla simu ulimuona akibandika kikaratasi
Shahidi: Sikumwambia
Wakili: Kazi ya kuzuia uhalifu ni yako au polisi
Shahidi: Polisi
Wakili: Chakula alichokula Adamoo na wenzake nani alilipia
Shahidi: Kililipiwa na pesa za Freeman Mbowe
Wakili: Ulisema katika fedha ulizowapa wakina Adamoo walitoa kiasi flani kwaajili ya chakula
Shahid: Sikusema
Wakili: Unafahamu hakuna simu ya Mbowe hata moja iliyokamatwa
Shahidi: Sifahamu
Wakili: Wewe ulikuwa una mamlaka yoyote ya kiupelelezi zaidi ya kutoa taarifa?
Shahidi: Sina mamla ya kiupelelezi zaidi ya kuto taarifa
Wakili Kibatala: Mheshimiwa Jaji bado nina maswali kwa shahidi na kupitia ombi letu naomba tuahirishe kesi hadi kesho Februari Mosi, 2020 kwaajili ya kuendelea na Cross Examination.
Wakili Kidando: Hatuna pingamizi Mheshimiwa iIa tunaomba Shahidi kesho ajielekeze kwenye maeneo ambayo hayajaulizwa.
Jaji: Naahirisha kesi hii hadi kesho Februari Mosi 2022 kwaajili ya shahidi wa 12 kuendelea kuhojiwa na upande wa utetezi.
Shahidi unakumbushwa kuja kuendelea kutoa ushahidi wako washtakiwa mtaendelea kuwa chini ya uangalizi wa Magereza.