Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wanajeshi wafunga anga ya Niger

Wanajeshi Wafunga Anga Ya Niger Wanajeshi wafunga anga ya Niger

Mon, 7 Aug 2023 Chanzo: Bbc

Viongozi wa mapinduzi ya Niger wamefunga anga ya nchi hiyo, kwa hofu ya kuvamiwa kijeshi.

Tovuti ya ufuatiliaji wa safari za ndege Flightradar24 inaonyesha kuwa kwa sasa hakuna ndege katika anga ya Niger.

Jumuiya ya Kiuchumi ya kanda ya Afrika Magharibi, Ecowas, ilikuwa imeonya inaweza kutumia nguvu ikiwa Rais Mohamed Bazoum hatarejeshwa madarakani ifikapo 23:00 GMT siku ya Jumapili.

Msemaji wa jeshi la serikali ya Niger anasema kuwa wanajeshi wa Niger wako tayari kuilinda nchi hiyo.

Bw Bazoum alizuiliwa tarehe 26 Julai, na Jenerali Abdourahmane Tchiani, kamanda wa walinzi wa rais, baadaye akajitangaza kuwa kiongozi mpya.

Mapinduzi hayo ya kijeshi yamelaaniwa kimataifa, ikiwa ni pamoja na mkoloni wa zamani Ufaransa na mataifa mengine ya Umoja wa Ulaya, pamoja na Umoja wa Mataifa na Marekani.

Baada ya mkutano wa dharura nchini Nigeria, wakuu wa jeshi la Ecowas walisema siku ya Ijumaa kwamba wameandaa mpango wa kina wa uwezekano wa kutumia nguvu.

"Masuala yote kuhusu hatua yoyote ya kuingilia kati yameshafanyiwa kazi, ikiwa ni pamoja na rasilimali zote zinazohitajika, namna gani na lini tutapeleka Jeshi", alisema Abdel-Fatau Musa, Kamishna wa ECOWAS anayeshughulikia masuala ya kisiasa, amani na usalama

Na akaongeza: "Tunataka diplomasia ifanye kazi, na tunataka ujumbe uwafikie bayana [watawala wa Niger] kwamba tunawapa kila fursa ya kubadili walichofanya".

Ecowas ni jumuiya yabiashara ya kikanda ya nchi 15 za Afrika Magharibi, zikiwemo Nigeria, Senegal, Togo na Ghana.

Chanzo: Bbc
Related Articles: