Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mali, Burkina Faso kutuma ujumbe nchini Niger

Mali, Burkina Faso Kutuma Ujumbe Nchini Niger Mali, Burkina Faso kutuma ujumbe nchini Niger

Mon, 7 Aug 2023 Chanzo: Bbc

Mali imesema itatuma ujumbe wa pamoja na Burkina Faso nchini Niger kuonesha mshikamano wao.

Tangazo hilo linakuja siku moja baada ya majenerali, walionyakua mamlaka nchini Niger kukaidi agizo la kumrejesha madarakani rais aliyechaguliwa la sivyo wakabiliane na uwezekano wa kuingiliwa kwa silaha kutoka mataifa mengine ya Afrika Magharibi.

Wanajeshi hao walisema kuwa wamefunga anga ya Niger na wanajiandaa kutetea eneo lake.

Licha ya uamuzi huo wa mwisho, wanachama wa kikundi cha kikanda cha Ecowas wamegawanyika kuhusu kuchukua hatua za kijeshi.

Nigeria na Ivory Coast ni miongoni mwa zile zinazosisitiza kuwa ni lazima Rais Mohamed Bazoum arejeshwe madarakani.

Lakini serikali za kijeshi nchini Mali na Burkina Faso zimesema zinaunga mkono viongozi wa mapinduzi iwapo watashambuliwa.

Chanzo: Bbc
Related Articles: