Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan anatarajia kuanza ziara ya kikazi, mkoani Mwanza, kesho Juni 12, 2023, hadi Juni 15, 2023, ambapo atatembelea na kukagua miradi mbalimbali likiwemo daraja la Kigongo-Busisi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan anatarajia kuanza ziara ya kikazi, mkoani Mwanza, kesho Juni 12, 2023, hadi Juni 15, 2023, ambapo atatembelea na kukagua miradi mbalimbali likiwemo daraja la Kigongo-Busisi. Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Bw.Amos Makalla ambapo pia amesema, Rais Samia atahudhuria Tamasha la Utamaduni linalojulikana kama Bulabo, litakalofanyika katika eneo la Makumbusho la Bujora.