Menu ›
Habari
Mon, 3 Jul 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Rais Samia Suluhu Hassan ametengua uteuzi wa Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Mwanahamisi Munkunda na kumteua Mobhare Holmes Matinyi kuwa Mkuu wa Wilaya ya hiyo.
Pia ametengua uteuzi wa Mkuu wa Wilaya ya Kilindi Abel Yeji Busalama, na amemhamisha kituo Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Hashim Shaib Mgandilwa kwenda kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kilindi.
Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu imesema Rais Samia amemteua James Wilbert kuwa Mkuu wa Wilaya ya Tanga Mjini.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: