Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Alikiba alisota sana, hakuiamini Cinderela

Alikiba Hnnnn Alikiba alisota sana, hakuiamini Cinderela

Mon, 10 Jul 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Ngoma ya #Cinderela ya kwake Alikiba (@officialalikiba ) ndio wimbo uliomtambulisha kwenye soko la #BongoFleva na kumfungulia milango ya safari yake kwenye muziki huo ila unaambiwa Alikiba mwenyewe hakuwa anaiamini ngoma hiyo kabisa bali alikuwa anataka wimbo wa #NakshiNakshi ndio utoke kwanza

Dusko Dalla ambaye alikuwa meneja wa G Records (Studio iliyofanya wimbo wa Cinderella) amepiga stori na @yoram004 na kueleza namna Alikiba alivyokuwa akipinga wimbo huo kutoka

"Alikuwa anasema #NakshiNakshi ndio wimbo pendwa nyumbani kwao lakini nikamwambia wimbo wa Cinderella ndio wimbo wa kumtoa na sababu kwa kipindi kile pale studio walikuwa wakiniamini sana ilibidi wakubali ndio Cinderella ikatoka na ukawa wimbo mkubwa"

"Watu hawajui kuwa Alikiba Alisota sana kabla ya kutoka na alikuwa amerekodi nyimbo nyingi pale G Records."

Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: