Mon, 25 Jun 2018
Chanzo: bongo5.com
Mchezaji tennis raia wa Croatia, Marin Cilic amefanikiwa kutwaa ubingwa wa Fever Tree Championships baada ya kumshinda Novak Djokovic kwenye michuano hiyo mchezo uliyochezwa kwenye viwanja vya Queen’s Club hapo jana siku ya Jumapili.
Mcroatia huyo wikiendi hii amemfunga mchezaji namba moja kwa viwango vya ubora duniani, Novak na kutwaa ubingwa wake kwa jumla ya seti 5-7 7-6 (7-4) 6-3.
Cilic mwenye umri wa miaka 29 amefanikiwa kuchukua taji hilo kwa mara ya pili mara baada ya kumshinda, Feliciano Lopez .
Loading...
Chanzo: bongo5.com