Mchezaji tennis namba moja kwa viwango vya ubora nchini Uingereza mwanadada, Johanna Konta ameondolewa kwenyemichuano ya Australia Open baada ya kufungwa na mchezaji anaeshikilia nafasi 123 duniani, Bernarda Pera.
Johanna Konta ameshinda michezo mitatu pekee kati ya 11 aliyocheza
Mmarekani, Bernarda Pera amemshinda Konta kwa jumla ya seti 6-4 7-5 katika kipindi cha pili cha mchezo.
Mara baada ya kutolewa katika mashindano hayo Konta amesema “Ni jambo la kusisimua lakini tunaendelea vizuri na benchi langu la ufundi, siji sikii vizuri lakini kwa namna yoyote lazima nikubali matokeo,”Konta.
Konta ameongeza “Nimecheza kila namna mpaka kufikia pale kwa hakika sikuhitaji rejea nyumbani mapema.”
Bernarda Pera akitengeneza pointi 17 dhidi ya mbili pekee za Konta