Tue, 12 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Baada ya jina la Percy Tau kukosekana kwenye kikosi cha timu ya Taifa ya Afrika Kusini, Kilichoitwa kwa ajili ya kujiandaa na michezo ya kirafiki.
Kocha wa Afrika Kusini Hugo Broos ameeleza ni kwa nini ameamua kumuacha Staa huyo anayekipiga katika klabu ya Al Ahly;
"Nilisema 'hapana' kwa Percy Tau,Kaa Misri. Ukija kwa michezo ya kirafiki, ukicheza mchezo mbaya, itaanza tena [kelele kutoka kwa mashabiki]. Kwa hivyo hiyo ndiyo sababu Percy hayuko pamoja nasi. Sitaki kumuua. Ilitosha, baada ya AFCON. Kwa hivyo atakuwa tayari tena mnamo Juni. Na nitamuona Percy Tau mpya.”
Chanzo: www.tanzaniaweb.live