Tue, 1 Nov 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Aliyekuwa kocha wa Simba SC, Zoran Maki anaendelea kufanya vizuri kwenye ligi kuu Misri baada ya jana kuiongoza klabu yake ya Al Ittihad kutoka nyuma 1-0 na kushinda 3-1 dhidi ya El Geish.
Al Ittihad ipo kileleni mwa msimamo wa Ligi kuu Misri ikiwa imefikisha alama 9 baada mechi tatu.
Al Ittihad ipo mbele ya Zamalek na Al Ahly ambazo zina alama 6 kila mmoja lakini Ittihad ikiwa imecheza mchezo mmoja zaidi.
Ndiyo timu aliyofunga magoli mengi zaidi huku ikiruhusu bao moja.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live