Tue, 28 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Nyota wa zamani wa Barcelona, PSG, Manchester United na timu ya Taifa ya Sweden Zlatan Ibrahimovic ameeleza kuwa alikataa kwenda kufanya majaribio Arsenal.
Arsenal kipindi hicho ilikuwa chini ya kocha Arsene Wenger na Zlatan alikuwa na miaka 17 tu lakini alimwambia Wenger yeye sio mchezaji wa majaribio.
"Arsene Wenger aliniambia niende kufanya majaribio Arsenal nilipokuwa na miaka 17.Nilimwambia HAPANA Zlatan sio wa majaribio unatakiwa kujua mimi ni nani."
- Zlatan Ibrahimovic nyota wa zamani wa Barcelona, Manchester United, Psg na timu ya Taifa ya Sweden.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live