Tue, 23 Aug 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Zamalek imetwaa ubingwa wa Ligi kuu Misri baada ya wapinzani wao waliokuwa wakiwafuata kwa karibu Pyramids kupoteza mchezo wao ugenini dhidi ya Future FC.
Kwa kipigo hicho Pyramids alama 68 haiwezi kufikia alama 75 za Zamalek huku ikiwa imebakisha mechi mbili.
Zamalek imetwaa ubingwa wao wa pili mfululizo na wa 14 kihistoria ikiwa imebakisha mechi tatu pazia la Ligi kuu Nchini humo kufungwa.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live