Kocha wa Namungo, Papaa Mwinyi Zahera anafichua kuwa wakati akiwa kocha wa Yanga aliwahi kumpendekeza Matampi Ley asajiliwe lakini kutokana na hali ya kiuchumi wa wakati huo dili hilo likashindikana.
“Wakati nikiwa Yanga tulipokuwa tunapiga hesabu za kusajili kipa mzuri wa maana jina la kwanza lilikuwa ni Matampi, lakini kutokana na hali ya fedha wakati huo viongozi wakashindwa kumalizana naye.”
Hivyo wakamuomba asubiri kwanza wakusanye fedha lakini baada ya muda akapata ofa kubwa ya kwenda Saudi Arabia kwa klabu ya Al-Ansar iliyomuwekea fedha nyingi baada ya kumkosa ndio tukaenda kumchukua yule kipa wa Kenya Farouk Shikhalo.