GUMZO kubwa mjini Geita kwa sasa ni juu ya usajili wa nyota wa zamani wa Yanga na Polisi Tanzania, Kelvin Yondani, ambaye amesaini dili la mwaka mmoja Geita Gold, mkataba utakaomfanya kuziba safu ya ulinzi sambamba na Juma Nyosso ambaye tayari ameingia kwenye klabu hiyo.
GUMZO kubwa mjini Geita kwa sasa ni juu ya usajili wa nyota wa zamani wa Yanga na Polisi Tanzania, Kelvin Yondani, ambaye amesaini dili la mwaka mmoja Geita Gold, mkataba utakaomfanya kuziba safu ya ulinzi sambamba na Juma Nyosso ambaye tayari ameingia kwenye klabu hiyo. Akizungumza na Championi Ijumaa, Ofisa Habari wa Geita Gold, Hemed Kivuyo, amesema, ni kweliYondani ataungana na Juma Nyosso msimu huu baada ya kusaini mkataba wa mwaka mmoja, kwani wao wameamua kutengeneza ukuta wa kudumu ili waweze kufikia malengo yao.